Psalms 84

Kuionea Shauku Nyumba Ya Mungu

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Gitithi. Zaburi Ya Wana Wa Kora)


1 aEe Bwana Mwenye Nguvu Zote,
makao yako yapendeza kama nini!

2 bNafsi yangu inatamani sana,
naam, hata kuona shauku,
kwa ajili ya nyua za Bwana;
moyo wangu na mwili wangu
vinamlilia Mungu Aliye Hai.


3 cHata shomoro amejipatia makao,
mbayuwayu amejipatia kiota
mahali awezapo kuweka makinda yake:
mahali karibu na madhabahu yako,
Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote,
Mfalme wangu na Mungu wangu.

4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako,
wanaokusifu wewe daima.


5 dHeri wale ambao nguvu zao ziko kwako,
na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.

6 eWanapopita katika Bonde la Baka,
Yaani Bonde la Vilio.

hulifanya mahali pa chemchemi,
pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.
Au: baraka.


7 hHuendelea toka nguvu hadi nguvu,
hadi kila mmoja afikapo
mbele za Mungu huko Sayuni.


8 iEe Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu;
nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.

9 jEe Mungu, uitazame ngao yetu,
mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.


10 kSiku moja katika nyua zako ni bora
kuliko siku elfu mahali pengine;
afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu
kuliko kukaa katika mahema ya waovu.

11 lKwa kuwa Bwana ni jua na ngao,
Bwana hutoa wema na heshima;
hakuna kitu chema anachowanyima
wale ambao hawana hatia.


12 mEe Bwana Mwenye Nguvu Zote,
heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
Copyright information for SwhKC